Jumapili, 18 Desemba 2016

KILIMO CHA UMWAGILIAJI KATA YA BUPIGU

BUPIGU WATUMIA VEMA MTO MTUMBISI
Badala ya kusubiri mvua zinyeshe ndipo waingie mashambani,wakazi wa kijiji cha Bupigu wilayani Ileje mkoa wa Songwe wamejiingiza katika kilimo cha umwagiliaji wakati wa kiangazi hali inayowapunguzia makali ya maisha.

Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wetu umebaini juu ya uwepo wa mashamba madogo madogo ya mahindi, magimbi, mpunga, miwa, mbogamboga, ufugaji samaki na utunzaji wa mazingira.

Wakulima hao walieleza kuwa licha ya kunufaika na kilimo hicho kinachowapunguzia makali ya maisha  kumekuwa na tatizo la soko kwa mazao wanayozalisha hususani mbogamboga.
Kijana akiwa kwenye shamba la magimbi lililo kandokando ya Mto Mtumbisi.
Shamba la mahindi linalomwagiliwa Bupigu
Mama na watoto wake wakiandaa shamba la mpunga
Uoto wa asili aina ya makangaga uliotunzwa na kikundi cha Mkombozi
Mwanachama wa kikundi cha Mkombozi akiwa karibu na bwawa lao
Uoto wa asili wa kipekee katika kijiji hicho unaotunzwa vema usitoweke

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni