Jumatano, 30 Novemba 2016

WILAYA YA ILEJE YATAKIWA KUJIPANGA KUPAMBANA NA MAAMBUKIZI DHIDI YA VVU NA UKIMWI


Katibu Tawala  wa Wilaya ya Ileje akifungua kikao cha kupanga mikakati ya kupunguza maambukizi mapya ya VVU na UKIMWI.

WILAYA YA ILEJE YATAKIWA KUJIPANGA DHIDI YA VVU NA UKIMWI
Na;Daniel Mwambene: Songwe

Katika  kupunguza maambukizi  mapya ya VVU na UKIMWI makundi mbalimbali wilayani Ileje yametakiwa kuchukua hatua za dhati katika kulikabiri janga hili ambalo lilishatangazwa na Awamu ya Tatu.

Hayo yalisemwa na wawakilishi wa makundi mbalimbali waliokuwa wakichangia kwenye kikao cha kupanga mikakati ya kupunguza maambukizi mapya katika wilaya hiyo kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri .

Mratibu wa TACAIDS mikoa ya Songwe na Mbeya Emamanuel Petro akisoma taarifa ya UKIMWI kitaifa na kimkoa aliwataka wajumbe hao kuwa na mkakati itakayokwenda sambamba na mikakati ya kimkoa  na kitaifa.

Henry Kayuni Mwenyekiti wa  Muungano wa Vikundi vya WAVIU wilayani Ileje aliwataka wananchi wote kujiepusha na unyanyapaa kwa wenye VVU na kuwataka watu wenye maambukizi hayo kujitangaza ili kuiokoa jamii badala ya kujificha wakiendelea kuambukiza.

Naye mwakilishi wa makundi ya dini katika mafunzo hayo Shekh wa wilaya hiyo Khamiss Simbeye aliwataka wakazi wa wilaya hiyo kushikilia mafunzo ya dini zao.

Mwenyekiti wa Kamati ya UKIMWI ya Halmashauri ya Wilaya hiyo Mh.Diwani Gwalusako Kapesa aliwataka wanafunzi ambao wapo majumbani baada ya shule kufunga wasitumie muda huo kujihusisha na vitendo vya ngono kwa kutumia mwanya kuwa mbali na sheria za shule.

Akifunga mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Najum Tekka aliwataka walimu wa shule za msingi na sekondari kuunda klabu za mapambano dhidi ya UKIMWI.


Tangu serikali ianzishe Sera ya UKIMWI ya mwaka 2001 maambukizi yamekuwa  yakipungua kutokana na mikakati inayotoa elimu kuanzia ngazi ya familia hadi Taifa

Mratibu wa TACAIDS mikoa ya Songwe na Mbeya Emmanuel Petro akiwezesha katika kikao hicho.

Kaimu Mkurugenzi Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Ileje Bi; Nujum Tekka akifunga kikao hicho.

Jumanne, 29 Novemba 2016

MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA DARASA LA SABA 2016 YATANGAZWA RASMI


MKOA WA SONGWE KUVALIA NJUGA  SEKTA YA ELIMU
Na;Daniel Mwambene, Songwe
Wakati ya kitangazwa matokeo jumla ya Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi Tanzania, viongozi wa wilaya za mkoa wa Songwe wameahidi kufanya vema katika mwaka ujao ili kuondokana na aibu ya kuwa miongoni mwa mikoa 10 ya mwisho.

Ahadi hizo zilitolewa katika ukumbi wa sekondari ya Vwawa wakati Kamati ya Mkoa ya Uendeshaji wa Mitihani  ilipokuwa ikitoa matokeo jumla  kwa viongozi wa Halmashauri zote tano za mkoa huo.
Akisoma matokeo hayo Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye ni Katibu Tawala wa Mkoa huo Eliya Ntandu aliwambia viongozi wa wilaya hizo kuwa mkoa wao umekuwa miongoni mwa mikoa 10 ambayo haikufanya vizuri.

Aliongeza kuwa hali hiyo imechangiwa na kufanya vibaya kwa kila wilaya ambako pia kulichangiwa na ufaulu duni wa shule moja moja ambao unagusa wadau mbalimbali wa elimu.

Katika matokeo hayo Halmashauri  ya Mji wa Tunduma imekuwa kinara, ikifuatiwa na Mbozi, huku nafasi  ya  tatu  ikikaliwa na Ileje, ya  nne  Songwe na mkiani ipo wilaya ya Momba.
Shule ya binafsi ya Ilasi imeonekana kufanya vizuri baada ya kutoa mwanafunzi wa kwanza kimkoa huku shule ya msingi Kambarage ya Hamashauri ya Wilaya ya Songwe ikiwa haina mwanafunzi hata mmoja atakayekwenda sekondari.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje Mh. Ubatizo Songa alitoa wito kwa Wanasongwe kutofurahia hali hiyo  na kuahidi kujipanga upya ili kuachana na kuondokana hiyo.
Aliongeza kuwa,upya wa mkoa kisiwe kisingizio cha kufanya mambo vibaya yanayoleta matokeo duni na kuuabisha mkoa.

Kauli hiyo, iliungwa mkono na Mwenyekiti  Kamati ya Uendeshaji Mitihani alipokuwa akifunga kika hicho alipowataka viongozi kwenda sehemu kwenye vituo vyao vya kazi ili kubaini mapungufu yaliyojitokeza kna kuyatautia ufumbuzi kulingana na mazingira ya kila halmashauri.


Mkoa wa Songwe ulianzishwa mwanzoni mwa mwaka huu ukiwa umemegwa toka mkoa wa Mbeya ni miongoni mwa mikoa mipya ya Tanzania iliyoanzishwa miaka ya hivi karibuni hapa nchini,mikoa mingine ni  Njombe,Simiyu,Geita na Katavi.

Viongozi wa mkoa wa wa Songwe wakijiandaa  kutoa matokeo  jumla ya mkoa ya Kumaliza Elimu ya Msingi 2016.

.Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe  akitoa maagizo wakati wa kufunga kikao hicho

Kaimu Afisa Elimu wa mkoa wa Songwe akizungumza na wajumbe wa kikao hicho.

Mh. Mkuu wa Wilaya ya Ileje akichangia

Mh. Mwenyeki wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje akiongea

Wajumbe toka Halmashauri ya wilaya ya Mbozi

Wajumbe toka Halmashauri ya Wilaya ya Momba

HOSPITALI YA WILAYA YA ILEJE YAPATA MSAADA WA MASHUKA


HOSPITALI YA WILAYA YA ILEJE YAPATA MSAADA WA MASHUKA
Na;Daniel Mwambene,Songwe
Katika kukabiliana na tatizo la uhaba wa vifaa mbalimbali,hospitali ya Itumba imepokea mashuka 200 kutoka kwa mbunge wa  Jimbo la Uchaguzi la Ileje ikiwa ni sehemu ya mashuka 600  yatakayotolewa na mbunge huyo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi mashuka hayo, Katibu wa  mbunge Deo Mulungu alisema kuwa mashuka mengine 400  yatakabidhiwa mara yatakapofikishwa jimboni humo siku chache zijazo ,hivyo kukamilisha jumla ya mashuka 600.

Katibu huyo alieleza kuwa,mafanikio hayo yamefikiwa kutokana na juhudi za Mh.mbunge katika kutafuta wadau mbalimbali walio tayari kuchangia maendeleo ya wilaya hiyo.

Akipokea msaada huo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Haji  Mnasi alipongeza juhudi hizo na kuahidi kusimamia matumizi sahihi ya mashuka hayo na kuwapunguzia kero wagonjwa amboa huhitaji faraja muda wote wawapo hospitalini.

Kaimu Mganga Mkuu wa  Wilaya hiyo Rowland Mroso akishukuru kwa niaba ya watumishi wa hospitali hiyo aliahidi kutunza mashuka hayo kwa mujibu wa taratibu za afya na aliomba kutochoka kutoa misaada pale mbunge huyo atakapoombwa tena.

Hata hivyo,bado hospitali hiyo inakabiliwa na matatizo lukuki ikiwemo kukosa mtaalam wa  kutumia mashine ya x-ray ambayo ilishanunuliwa.


Tangu kupewa kibali cha kuwa hospitali ya wilaya  wananchi wa tarafa ya Bulambya wamepunguziwa kero ya muda mrefu ambapo hapo awali walilazimika kusafiri hadi hospitali ya Isoko zaidi ya kilometa 60 au kwenda nchi jirani ya Malawi. 

Kaimu Mganga Mkuu akimshurukuru Katibu wa Mh.Mbunge

Maboksi yenye mashuka 200 kwa ajili ya hospitali ya Itumba ambayo ni hospitali ya wilaya Ileje

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje Haji Mnasi (kushoto) akiwa  na Katibu wa Mh.mbunge(kulia) wakiwa katika eneo la hospitali kabla ya makabidhiano ya mashuka yaliyotolewa na Mh.Janet Mbene(mb).

Kaimu Mganga Mkuu Rowland Mroso (mwenye miwani) akishukuru kwa niaba ya watumishi wa hospitali hiyo na kuahidi kuyatunza vema.

Mkurugenzi akishukuru baada ya kupokea msaada huo akiahidi kusimamamia matumizi yake

Mmoja wa watumishi wa hospitali hiyo Oscar Kaponda akishukuru kwa msaada huo na kuomba mbunge aendelee kutafuta wadau wanaoweza kusaidia vifaa vingine vinavyopungua ikwemo ‘’utra sound’

Jumatatu, 28 Novemba 2016

SIKU YA USAFI YA KIWILAYA JUMAMOSI


Mh. Mkuu wa Wilaya ya Ileje akiwapongeza Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wiaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya, Wakuu wa Idara na vitengo na wananchi kwa ujumla kwa kujitokeza kushiriki zoezi zima la kufanya usafi katika mji wa Isongole.

Mh. Mkuu wa Wilaya ameagiza kwa watumishi na wananchi wote kwa ujumla kuhakikisha kila siku ya jumamosi ya kila wiki wanafanya usafi wa mazingira wanayoishi na maeneo yao ya biashara kuanzia saa moja asubuhi hadi saa nne na mara baada ya muda huo, shughuli za kawaida ziendelee.

MAFUNZO YA USAJILI WA WATOTO WA CHINI YA MIAKA MITANO WA VYETI VYA KUZALIWA


Mafunzo ya utoaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa umri wa chini ya miaka mitano yaliyokuwa yanaendeshwa na wataalamu wa RITA kutoka makao makuu. Mafunzo haya yamefanyika tarehe 28/11/2016 katika ukumbi wa shule ya sekondari Itumba yakihusisha watendaji wa kazi zote 18 za Halmashauri ya Wilaya ya Ileje, wafanyakazi wa vituo vya afya na zahanati zote za serikali na binafsi katika wilaya ya Ileje.

Baada ya kutoa mafunzo wataalam hao waliweza kugawa simu moja moja kwa kila mtendaji wa kata na vituo vyote vya afya na zahanati isipokuwa kwa kata na vituo vya afya ambavyo havina mtandao wa Tigo.

Simu hizo zimesimikwa mfumo maalum wa RITA utakaotumika katika kufanya usajili wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa chini ya miaka mitano.

SARE YAWANYIMA RAHA MASHABIKI WA TIMU YA MWENGE


SARE YAWANYIMA  RAHA  MASHABIKI WA TIMU YA MWENGE
Na Daniel Mwambene,Songwe
Ikiwa inamalizia mchezo wake wa mwisho wa Ligi  Daraja la Tatu  Mkoa wa Songwe timu ya soka ya Mwenge Sports Club ya Ileje  imeshindwa  kuwapa raha mashabiki wake baada ya kutoka suluhu na timu ya Vwawa Town ya Wilaya ya Mbozi mkoani humu.

Ikiwa katika uwanja  wake wa nyumbani katika kiijiji cha Isongole mbele ya Mkuu wao  wa Wilaya Joseph Mkude  Mwenge ilishindwa kutumia nafasi kadhaa ilizozipata kutokana na umahili wa golikipa Michael Mwakatera wa timu ya Vwawa.

Licha ya kufika mara kadhaa langoni mwa Vwawa kwa kuipenya ngome ya Vwawa iliyokuwa ikongozwa na Juma Siame na Geofrey Kasebele, Mwenge ilishindwa kabisa kutikisa nyavu za maadui huku mashabiki wake waliokuwa wamefurika kwenye uwanja uliozungushiwa’ matrubai’wakiwa wamesimama kushangilia wakidhani kuwa  lilikuwa ni goli.
Licha ya kufanya mabadiliko kwa kila timu hadi dakika 90 zikikamilika si Mwenge wala Vwawa waliokuwa wamepata goli.

Matokeo haya yanaiwezesha Mwenge kufikisha pointi tisa kwenye kundi lake  ikiungana na timu ya Morning Star ya Tunduma wilayani Momba  na timu za makundi mengine ili kuingia katika hatua nyingine ya ligi ya mkoa huo

Akizungumza mara baada ya mchezo huo mmoja wa mashabiki ya timu hiyo,Zakaria Kyomo alisema kuwa  mchezo ulikuwa mzuri ila ladhaa yake ilipungua kutokana na kutopata goli.


Timu hii ni mojawapo ya timu kongwe wilayani Ileje timu zingine ni pamoja na Itumba Stars,Mbebe Rangers  na timu ya Uhuru toka kataLubanda.

Mh. Mkuu wa Wilaya ya Ileje akiwasili uwanjani kwa ajili ya kushuhudia mechi

Wachezaji wa timu ya Vwawa wakipasha kabla ya mechi kuanza

Mh. Mkuu wa Wilaya ya Ileje akiingia Uwanjani kushuhudia mchezo

Mh. Mkuu wa Wilaya Ileje alikagua wachezaji kabla ya Mechi kuanza

Mh. Mkuu wa Wilaya akitoa mawaidha kwa wachezaji kabla ya mchezo