Jumatano, 30 Novemba 2016

WILAYA YA ILEJE YATAKIWA KUJIPANGA KUPAMBANA NA MAAMBUKIZI DHIDI YA VVU NA UKIMWI


Katibu Tawala  wa Wilaya ya Ileje akifungua kikao cha kupanga mikakati ya kupunguza maambukizi mapya ya VVU na UKIMWI.

WILAYA YA ILEJE YATAKIWA KUJIPANGA DHIDI YA VVU NA UKIMWI
Na;Daniel Mwambene: Songwe

Katika  kupunguza maambukizi  mapya ya VVU na UKIMWI makundi mbalimbali wilayani Ileje yametakiwa kuchukua hatua za dhati katika kulikabiri janga hili ambalo lilishatangazwa na Awamu ya Tatu.

Hayo yalisemwa na wawakilishi wa makundi mbalimbali waliokuwa wakichangia kwenye kikao cha kupanga mikakati ya kupunguza maambukizi mapya katika wilaya hiyo kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri .

Mratibu wa TACAIDS mikoa ya Songwe na Mbeya Emamanuel Petro akisoma taarifa ya UKIMWI kitaifa na kimkoa aliwataka wajumbe hao kuwa na mkakati itakayokwenda sambamba na mikakati ya kimkoa  na kitaifa.

Henry Kayuni Mwenyekiti wa  Muungano wa Vikundi vya WAVIU wilayani Ileje aliwataka wananchi wote kujiepusha na unyanyapaa kwa wenye VVU na kuwataka watu wenye maambukizi hayo kujitangaza ili kuiokoa jamii badala ya kujificha wakiendelea kuambukiza.

Naye mwakilishi wa makundi ya dini katika mafunzo hayo Shekh wa wilaya hiyo Khamiss Simbeye aliwataka wakazi wa wilaya hiyo kushikilia mafunzo ya dini zao.

Mwenyekiti wa Kamati ya UKIMWI ya Halmashauri ya Wilaya hiyo Mh.Diwani Gwalusako Kapesa aliwataka wanafunzi ambao wapo majumbani baada ya shule kufunga wasitumie muda huo kujihusisha na vitendo vya ngono kwa kutumia mwanya kuwa mbali na sheria za shule.

Akifunga mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Najum Tekka aliwataka walimu wa shule za msingi na sekondari kuunda klabu za mapambano dhidi ya UKIMWI.


Tangu serikali ianzishe Sera ya UKIMWI ya mwaka 2001 maambukizi yamekuwa  yakipungua kutokana na mikakati inayotoa elimu kuanzia ngazi ya familia hadi Taifa

Mratibu wa TACAIDS mikoa ya Songwe na Mbeya Emmanuel Petro akiwezesha katika kikao hicho.

Kaimu Mkurugenzi Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Ileje Bi; Nujum Tekka akifunga kikao hicho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni