Jumanne, 29 Novemba 2016

HOSPITALI YA WILAYA YA ILEJE YAPATA MSAADA WA MASHUKA


HOSPITALI YA WILAYA YA ILEJE YAPATA MSAADA WA MASHUKA
Na;Daniel Mwambene,Songwe
Katika kukabiliana na tatizo la uhaba wa vifaa mbalimbali,hospitali ya Itumba imepokea mashuka 200 kutoka kwa mbunge wa  Jimbo la Uchaguzi la Ileje ikiwa ni sehemu ya mashuka 600  yatakayotolewa na mbunge huyo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi mashuka hayo, Katibu wa  mbunge Deo Mulungu alisema kuwa mashuka mengine 400  yatakabidhiwa mara yatakapofikishwa jimboni humo siku chache zijazo ,hivyo kukamilisha jumla ya mashuka 600.

Katibu huyo alieleza kuwa,mafanikio hayo yamefikiwa kutokana na juhudi za Mh.mbunge katika kutafuta wadau mbalimbali walio tayari kuchangia maendeleo ya wilaya hiyo.

Akipokea msaada huo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Haji  Mnasi alipongeza juhudi hizo na kuahidi kusimamia matumizi sahihi ya mashuka hayo na kuwapunguzia kero wagonjwa amboa huhitaji faraja muda wote wawapo hospitalini.

Kaimu Mganga Mkuu wa  Wilaya hiyo Rowland Mroso akishukuru kwa niaba ya watumishi wa hospitali hiyo aliahidi kutunza mashuka hayo kwa mujibu wa taratibu za afya na aliomba kutochoka kutoa misaada pale mbunge huyo atakapoombwa tena.

Hata hivyo,bado hospitali hiyo inakabiliwa na matatizo lukuki ikiwemo kukosa mtaalam wa  kutumia mashine ya x-ray ambayo ilishanunuliwa.


Tangu kupewa kibali cha kuwa hospitali ya wilaya  wananchi wa tarafa ya Bulambya wamepunguziwa kero ya muda mrefu ambapo hapo awali walilazimika kusafiri hadi hospitali ya Isoko zaidi ya kilometa 60 au kwenda nchi jirani ya Malawi. 

Kaimu Mganga Mkuu akimshurukuru Katibu wa Mh.Mbunge

Maboksi yenye mashuka 200 kwa ajili ya hospitali ya Itumba ambayo ni hospitali ya wilaya Ileje

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje Haji Mnasi (kushoto) akiwa  na Katibu wa Mh.mbunge(kulia) wakiwa katika eneo la hospitali kabla ya makabidhiano ya mashuka yaliyotolewa na Mh.Janet Mbene(mb).

Kaimu Mganga Mkuu Rowland Mroso (mwenye miwani) akishukuru kwa niaba ya watumishi wa hospitali hiyo na kuahidi kuyatunza vema.

Mkurugenzi akishukuru baada ya kupokea msaada huo akiahidi kusimamamia matumizi yake

Mmoja wa watumishi wa hospitali hiyo Oscar Kaponda akishukuru kwa msaada huo na kuomba mbunge aendelee kutafuta wadau wanaoweza kusaidia vifaa vingine vinavyopungua ikwemo ‘’utra sound’

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni