Jumatatu, 28 Novemba 2016

SARE YAWANYIMA RAHA MASHABIKI WA TIMU YA MWENGE


SARE YAWANYIMA  RAHA  MASHABIKI WA TIMU YA MWENGE
Na Daniel Mwambene,Songwe
Ikiwa inamalizia mchezo wake wa mwisho wa Ligi  Daraja la Tatu  Mkoa wa Songwe timu ya soka ya Mwenge Sports Club ya Ileje  imeshindwa  kuwapa raha mashabiki wake baada ya kutoka suluhu na timu ya Vwawa Town ya Wilaya ya Mbozi mkoani humu.

Ikiwa katika uwanja  wake wa nyumbani katika kiijiji cha Isongole mbele ya Mkuu wao  wa Wilaya Joseph Mkude  Mwenge ilishindwa kutumia nafasi kadhaa ilizozipata kutokana na umahili wa golikipa Michael Mwakatera wa timu ya Vwawa.

Licha ya kufika mara kadhaa langoni mwa Vwawa kwa kuipenya ngome ya Vwawa iliyokuwa ikongozwa na Juma Siame na Geofrey Kasebele, Mwenge ilishindwa kabisa kutikisa nyavu za maadui huku mashabiki wake waliokuwa wamefurika kwenye uwanja uliozungushiwa’ matrubai’wakiwa wamesimama kushangilia wakidhani kuwa  lilikuwa ni goli.
Licha ya kufanya mabadiliko kwa kila timu hadi dakika 90 zikikamilika si Mwenge wala Vwawa waliokuwa wamepata goli.

Matokeo haya yanaiwezesha Mwenge kufikisha pointi tisa kwenye kundi lake  ikiungana na timu ya Morning Star ya Tunduma wilayani Momba  na timu za makundi mengine ili kuingia katika hatua nyingine ya ligi ya mkoa huo

Akizungumza mara baada ya mchezo huo mmoja wa mashabiki ya timu hiyo,Zakaria Kyomo alisema kuwa  mchezo ulikuwa mzuri ila ladhaa yake ilipungua kutokana na kutopata goli.


Timu hii ni mojawapo ya timu kongwe wilayani Ileje timu zingine ni pamoja na Itumba Stars,Mbebe Rangers  na timu ya Uhuru toka kataLubanda.

Mh. Mkuu wa Wilaya ya Ileje akiwasili uwanjani kwa ajili ya kushuhudia mechi

Wachezaji wa timu ya Vwawa wakipasha kabla ya mechi kuanza

Mh. Mkuu wa Wilaya ya Ileje akiingia Uwanjani kushuhudia mchezo

Mh. Mkuu wa Wilaya Ileje alikagua wachezaji kabla ya Mechi kuanza

Mh. Mkuu wa Wilaya akitoa mawaidha kwa wachezaji kabla ya mchezo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni