Jumanne, 29 Novemba 2016

MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA DARASA LA SABA 2016 YATANGAZWA RASMI


MKOA WA SONGWE KUVALIA NJUGA  SEKTA YA ELIMU
Na;Daniel Mwambene, Songwe
Wakati ya kitangazwa matokeo jumla ya Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi Tanzania, viongozi wa wilaya za mkoa wa Songwe wameahidi kufanya vema katika mwaka ujao ili kuondokana na aibu ya kuwa miongoni mwa mikoa 10 ya mwisho.

Ahadi hizo zilitolewa katika ukumbi wa sekondari ya Vwawa wakati Kamati ya Mkoa ya Uendeshaji wa Mitihani  ilipokuwa ikitoa matokeo jumla  kwa viongozi wa Halmashauri zote tano za mkoa huo.
Akisoma matokeo hayo Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye ni Katibu Tawala wa Mkoa huo Eliya Ntandu aliwambia viongozi wa wilaya hizo kuwa mkoa wao umekuwa miongoni mwa mikoa 10 ambayo haikufanya vizuri.

Aliongeza kuwa hali hiyo imechangiwa na kufanya vibaya kwa kila wilaya ambako pia kulichangiwa na ufaulu duni wa shule moja moja ambao unagusa wadau mbalimbali wa elimu.

Katika matokeo hayo Halmashauri  ya Mji wa Tunduma imekuwa kinara, ikifuatiwa na Mbozi, huku nafasi  ya  tatu  ikikaliwa na Ileje, ya  nne  Songwe na mkiani ipo wilaya ya Momba.
Shule ya binafsi ya Ilasi imeonekana kufanya vizuri baada ya kutoa mwanafunzi wa kwanza kimkoa huku shule ya msingi Kambarage ya Hamashauri ya Wilaya ya Songwe ikiwa haina mwanafunzi hata mmoja atakayekwenda sekondari.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje Mh. Ubatizo Songa alitoa wito kwa Wanasongwe kutofurahia hali hiyo  na kuahidi kujipanga upya ili kuachana na kuondokana hiyo.
Aliongeza kuwa,upya wa mkoa kisiwe kisingizio cha kufanya mambo vibaya yanayoleta matokeo duni na kuuabisha mkoa.

Kauli hiyo, iliungwa mkono na Mwenyekiti  Kamati ya Uendeshaji Mitihani alipokuwa akifunga kika hicho alipowataka viongozi kwenda sehemu kwenye vituo vyao vya kazi ili kubaini mapungufu yaliyojitokeza kna kuyatautia ufumbuzi kulingana na mazingira ya kila halmashauri.


Mkoa wa Songwe ulianzishwa mwanzoni mwa mwaka huu ukiwa umemegwa toka mkoa wa Mbeya ni miongoni mwa mikoa mipya ya Tanzania iliyoanzishwa miaka ya hivi karibuni hapa nchini,mikoa mingine ni  Njombe,Simiyu,Geita na Katavi.

Viongozi wa mkoa wa wa Songwe wakijiandaa  kutoa matokeo  jumla ya mkoa ya Kumaliza Elimu ya Msingi 2016.

.Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe  akitoa maagizo wakati wa kufunga kikao hicho

Kaimu Afisa Elimu wa mkoa wa Songwe akizungumza na wajumbe wa kikao hicho.

Mh. Mkuu wa Wilaya ya Ileje akichangia

Mh. Mwenyeki wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje akiongea

Wajumbe toka Halmashauri ya wilaya ya Mbozi

Wajumbe toka Halmashauri ya Wilaya ya Momba

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni