Alhamisi, 1 Desemba 2016

ZOEZI LA UPIMAJI WA UWINGI WA MAJI KATIKA VISIMA LA PAMBA MOTO


Katika kuhakikisha Halmashauri ya Wilaya ya Ileje inakua na uhakika katika suala zima na upatikanaji wa kwa vijiji vyote ndani ya wilaya. Leo Idara ya Maji ikiongozwa na mkuu wa idara hiyo Eng. Marco Kalamu alisaidiana na wasaidizi wake akiwemo Eng. Briton walikuwa katika kijiji cha Mangwina kilichopo kata ya Bupigu.

Lengo la ziara yao lilikuwa ni kwenda kupima uwingi wa maji katika kisima hicho ili kujua uwezo wa kisima kabla ya kufunga pampu ya maji itakayokuwa inatumia solar.

Zoezi hilo linatarajiwa kufanyika pia katika kijiji cha Mapogoro kilichopo katika katika kata ya Mbebe. Hii yote ni katika harakati za kupambana na tatizo la uhaba wa maji katika baadhi ya vijiji katika wilaya ya Ileje

Eng. Marko Kalamu Mkuu wa Idara ya Maji  akifuatilia kwa makini upimaji wa uwingi wa maji katika kisima cha maji cha kijiji cha Mangwina.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni