Jumapili, 18 Desemba 2016

MAANDALIZI YA KIDATO CHA KWANZA 2016

ILEJE YAJIANDAA KUPOKEA KIDATO CHA KWANZA 2017
Na;Daniel Mwambene, Songwe
Zikiwa zimebaki takribani wiki tatu ili kuanza mwaka mpya wa masomo kwa shule za msingi na sekondari hapa nchini wilaya ya Ileje mkoani hapa imeanza kuandaa mazingira ya kuwapokea wanafunzi hao.

Katika kufanya hivyo,viongozi wa Halmshauri ya wilaya hiyo wamekuwa wakitembelea shule za sekondari zilizopo wilayani humo ili kujiridhisha,ambapo hivi karibuni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya aliongoza baadhi ya watendaji wake kutembelea shule zilizo na miradi ya SEDP.

Mkurugenzi huyo, Bw.Haji Mnasi aliweza kutembelea shule za sekondari Itale, Luswisi, Msomba na Bupigu zenye miradi ya ujenzi wa nyumba za walimu zitakazokuchukua familia sita (Six in One).

Pia kwenye baadhi ya shule hizo kuna miradi ya ujenzi na ukarabati wa vyumba vya madarasa na ujenzi wa vyoo vya kisasa.

Akizungumza na wakandarasi  katika shule alizotembelea mkurugenzi huyo aliwataka kumalizia kazi hiyo  mapema zaidi ili kuyafanya mazingira ya shule kuwa rafiki kwa walimu na wanafunzi yakienda sambamba na uwepo wa umeme unaosambazwa na serikali vijijini.

Naye mwandisi wa ujenzi wa wilaya hiyo, Bw.Hatibu Nunu aliwataka wakandarasi hao kufanya marekebisho katika maeneo aliyokuwa amebaini kukosewa kulingana na mikataba ya ujenzi waliyotiliana saini.
Sehemu ya uani ya nyumba ya walimu sekondari ya Itale(SEDP)
Mafundi wakiendelea na kazi kwenye jingo la madarasa sekondari ya Itale(SEDP)
Vyoo vinavyoengwa na SEDP sekondari ya Itale
Vyoo vilivyokuwepo kabla ya mradi wa SEDP

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni