Alhamisi, 12 Januari 2017

ILEJE WAADHIMISHA MAPINDUZI YA ZANZIBAR KWA KUPANDA MITI

 Mkuu wa Wilaya ya Ileje Mh.Joseph Mkude akielekea eneo la upandaji miti

Na;Daniel Mwambene, Ileje
Watumishi wa Serikali Kuu, Serikali za Mitaa na wadau wengine wilayani Ileje wamesherekea Sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kupanda miti ili kuilinda wilaya hiyo dhidi ya ukame.

Zoezi hilo lililoongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mh.Joseph Mkude pia lilihusisha watendaji wa ofisi yake, Kamati ya Ulinzi na Usalama, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Wakuu wa Idara na Vitengo, Wahudumu wa Ofisi pamoja na wadau wengine

Katika zoezi hilo Zaidi ya miti 200 iliyonunuliwa na Ofisi ya Mkurugenzi ilipandwa katika eneo la boma jipya lililopo mjini Itumba ambayo ni makao makuu ya wilaya hiyo.

Akizungumza mara baada ya zoezi hilo kukamilika Mkuu wa Wilaya hiyo aliwataka watumishi kuwa na mwitikio chanya katika matukio kama hayo akisema kuwa yanaashiria uzalendo kwa Taifa.

‘’Ndugu zangu watumishi nawashukuru kuitikia wito wangu lakini naomba msichukulie matukio kama haya kuwa ni adhabu bali ni sehemu ya kazi inayotakiwa kukuongezea furaha katika moyo wako’’,alilisisitiza Mh. Mkude.

Alisema kuwa miti mingi iliyopo katika maeneo yanayotuzunguka haikufikia hapo bila juhudi za watu kufanyika kwa kuipanda au kuitunza,tabia ambazo alisema haina budi kuenziwe kwa kupanda miti kama zoezi lilivyofanyika.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo  Bw Haji Mnasi aliiahidi kusimama zoezi hilo na kuwataka viongozi wa halmashauri kufanya ukaguzi wa kila sehemu watakayotembelea ndani ya wilaya hiyo ili kujua utekeleji wa wa zoezu la upandaji miti unavyokwenda.

Mnasi aliongeza kuwa ni wajibu wa  kila kiongozi wa ngazi ya halmashauri hadi kitongoji kuhakikisha anafuatilia zoezi hilo kwa walio chini yake na mwananchi mmoja mmoja.

Mkuu wa Polisi wa Wilaya hiyo Afande Fadhil Ishekazoba aliwataka wananchi kulinda miti iliyopandwa ili kuepukana na kufanya kazi ambayo haina matokeo chanya.

Alisema kuonesha kazi ilifanyika ni vema kuona ongezeko la miti inayokuwa katika maeneo mbalimbali  badala ya kuwa na idadi kubwa ya miti inayopandwa kila mwaka huku ikiishia kuliwa na mifugo pamoja na kuharibiwa na wanaokata kwaajili ya nishati ya kupikia.

Akizungumza kwa niaba ya watumishi walioshiriki zoezi hilo Afisa Elimu Msingi Mwalimu Godwin Mkaruka aliahidi kuongeza idadi ya miti katika wilaya hiyo akitumia jeshi lake ambalo ni wanafunzi wakiongozwa na walimu wao

Alisema kuwa kila shule ilishaandaa kitalu cha miche tangu mwaka jana ukiwa ni utekelezaji wa agizo la Mkuu wa Mkoa huu wa Songwe Mh.Chiku Galawa aliyezitaka shule zote za msingi na sekondari kufanya hivyo.
 Katibu Tawala Wilaya ya Ileje Bi; Mary Joseph Marco akipanda mti
 Mmoja wa watumishi wa halmashauri akiwa kazini
 Mkuu wa Wilaya akipanda mti
 Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Ileje Haji Mnasi akishiriki kupanda miti
 Watumishi wa serikali wakishiriki zoezi hilo


 Washiriki wa upandaji miti wakifurahia hotuba fupi ya Mkuu wa Wilaya
 Mkuu wa Polisi(OCD) wa Wilaya ya Ileje Afande Fadhil Majjid Ishekazoba akizungumza na walioshiriki upandaji wa miti akisisiza kuitunza




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni