Jumapili, 1 Januari 2017

VIONGOZI WA SACCOS YA WALIMU ILEJE WATUMBULIWA

Na;Daniel Mwambene, Ileje - Songwe 

Viongozi walioweka mifukoni mwao SACCOS ya walimu Ileje watumbuliwa na uongozi wa mkoa wa Songwe ili kuiokoa isitoweke katika ramani ya vyama vya ushirika hapa nchini.

Hatimaye sintofahamu na kiza kinene kilichokuwa kinakikumba Chama cha Akiba na Mikopo cha Walimu wilayani Ileje kwa takribani miaka miwili kimepata mwanga baada ya viongozi waliokuwepo kuvuliwa madaraka kutokana na kanuni nyingi za uendeshaji kukiukwa huku SACCOS hiyo ikiendeshwa kama mradi wa mtu asiyekuwa makini.

Kung’olewa kwao kulitangazwa na Mrajisi wa Vyama vya Ushirika mkoani Songwe Marton Mtindya kwenye mkutano maalum uliofanyika kwenye ukumbi wa Mkuu wa Wilaya hiyo mjini Itumba ukiwaondoa mwenyekiti,katibu wake na baadhi ya wajumbe wa bodi kwa kupoteza sifa za uongozi.

Walion’golewa ni mwenyekiti Elimu Kaminyoge, katibu wake Alam Pwele na baadhi ya wajumbe wa bodi ambao kwa muda wote walikuwa wakiendesha chama kinyume na sheria.
Akisoma taarifa kwa wajumbe waliokuwa wamejaa jazba mlajisi wa mkoa huo Mtindya alitaja madhaifu kadha wa kadha yaliyofanywa na viongozi hao na kuuelekeza ushirika huo katika kifo cha milele wakisababisha watu kujiondoa uanachama kila uchapo badala ya kuongeza.

Mtindya aliyataja madhaifu hayo kuwa ni kutochangia kila mwezi kama katiba yao inayoelekeza,kukopa pesa bila kurejesha kila mwezi huku wengine kuwa na makato madogo tofauti na mkataba wa mkopo, mwenyekiti na katibu kuandika barua za kujiondoa uanachama kwa kupitishiana wao kwa wao katika makato ya shilingi 20,000/= ya kila mwezi pasipo kushirikisha viongozi wengene huku wakiwa na mikopo mikubwa isiyo na marejesho.

Alibainisha tuhuma zingine kuwa ni kushindwa kuitisha mikutano mikuu kwa miaka miwili mfulululizo sasa hali iliyosababisha wanachama kukosa taarifa za ushirika wao ambao ulikuwakimbilio la wengi na kuwa ushirika wa kuigwa wilayani humo kwamiaka kadha iliyopita.

Aliongeza kuwa kutokana na utendaji huo mbovu wastaafu,waliohama wilaya na waliojitoa uanachama SACCOS imeshindwa kuwapa sitahiki zao ambazo walizitunza kwamalengo maalum ,hivyo kuuchukulia ushirika kama sehemu ya utapeli  badala ya kuwa kimbilio,hali aliyoielezea kuwa haitavumliwa kwa SACCOS yoyote katika mkoa wa Songwe.

Mrajisi huo alipata wakati mgumu wakati wa kikao hicho kutokana na wanachama kuonesha hasira zao kwa viongozi wakieleza kutokuwa na imani nao kwa kutosikiliza shida zao kwa muda mrefu.

Pamoja na hali hiyo kuchangiwa na viongozi hao Mtindya alieleza kuwa matatizo yalianzia kwenye uongozi ulioondoka madarakani miaka miwili iliyopita ambapo walikuwa pia wakitoa pesa kwa wanachama pasipo kufuata taratibu zinazotakiwa.

Licha ya kuvuliwa nafasi zao za uongozi pia wametakiwa kujisalimisha kwa mwajiri wao ili kukubaliana ni jinsi gani watalipa pesa wanazodaiwa ama sivyo ifikapo mwishoni mwa mwezi Januari 2017 mishahara yao itazuiliwa kwa kile alichoeleza kuwa wamekenda kinyume na ilani ya Chama Cha Mapinduzi inayolenga kuinua ushirika.

Said Ngondo mmmoja wa walionufaika na ukopeshaji huo haramu aliueleza mkutano kuwa nikwelikatika kipindi hicho alikopeshwa pesa posipo kujaza mkataba wowote ingawa kwa imani yake aliendeleakurejesha kila mwezi.

Mjumbe mwingine mwalimu Alfred Mbukwa alinyoshea mkono pia baadhi ya watendaji wa Benki ya CRDB hasa mtu aliyekuwepo katika mkutano wa mwisho 2014 aliyemtaja kwa jina moja la Kayombo kuwa ana mchango wake katika kuifikisha pabaya SACCOS hiyo kwa vile alionekana kutetea watuhumiwa pale walponyoshewa vidole kuwa walikuwa wakiupeleka ushirika huo kusikojulikana.

Baada ya kuwang’oa vigogo hao, uliundwa uongozi wa mpito ukiongozwa na mwalimu Damas Masebo aliyekuwa Makamu Mwenyekiti, Said Ngondo akipewa umakamu Fabian Sigara akichukua nafasi ya Meneja.

Wajumbe wengine wa bodi ni Elias Bowa, Deogratius Mhume, Syoni Swila, Jose Songa na Lucian Yunga ambao kwa pamoja wamepewa dhamana ya kuhakikisha ushirika huo unarudi kwenye mstari na kuwa kimbilio la wengi.

Akizungumza mwishoni mwa mkutano huo aliyeondolewa kwenye uenyekiti mwalimu Elimu Kaminyoge aliwaeleza wajumbe kuwa hali hiyo ilichangiwa na hali mbaya aliyoikuta katika SACCOS ambapo tayari lilikuwa ni pakacha lililokuwa likivuja.

Akizungumza nje ya ukumbi huo, mmoja wa wajumbe wapya wa bodi hiyo mwalimu Deogratiuas Mhume alisema kuwa katika wakati huu, viongozi hawana budi kuchukua maamuzi maguu na ya haraka ili kuokoa watu wengi kama uongozi wa mkoa ulivyofanya ukishirikana na viongozi wa serilkali wa wilaya ya Ileje.

Alisema kuwa kilichokuwa ndani ya ushirika huo ni sawa na sumu ya nyoka ambaye dawa yake yaweza kuwa ni kuondolewa kwa kiungo kilichofikiwa nasumu ili isienee mwili mzima.

Mrajisi wa vyama vya ushirika mkoa wa Songwe Marton Mtindya (kulia) akituliza jazba zilizowapanda wanachama, kulia kwake ni mwenyekiti aliyetemwa mwalimu Elimu Kaminyoge

Mtindya akielezea kwa wanachama mapungufu yaliyobainika katika ukaguzi uliofanyika

Mwalimu Jose Songa akielezea jinsi viongozi wa SACCOS hiyo walivyochangia kuwaondolea matumaini wanachama wake

Mwalimu Alfred Mbukwa aliyesimama akielezea jinsi mmoja wa watumishi wa benki ya CRDB alivyochangia kulinda uovu ndani ya ushirika huo

Sehemu ya wanachama wa SACCOS hiyo wakiwa kwenye mkutano huo

Mwalimu Syoni Swila aliyenyosha mkono akichangia katika mkutano huo

Mwalimu Damas Masebo (maarufu kama Old Monkey) aliyepewa uenyekiti na kuhakikisha SACCOS inarudi kwenye mstari akionyesha sura ya kazi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni