Jumanne, 3 Januari 2017

VITUKO NDANI YA MTO SONGWE WILAYANI KYELA

Na;Daniel Mwambene Songwe
Waswahili husema kuwa” Macho hayana pazia”haya yalinikuta siku chache zilizopita nikielekea Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwila uliopo Ileje katika mkoa wa Songwe.

Macho yangu pekee hayakutosha kuweza kuona na kutunza kumbukumbu za kudumu juu ya mambo niliyoyaona katika safari ya kuelekea katika mgodi huo nililazimika kutumia kamera ili kila kitu kisiweze kupotea nikisafiri masaa kadha kutoka Itumbamakao makuu ya wilaya ya Ileje kwa kuzipita wilaya za Kyela na Rungwe na kurudi tena Itumba.

Mzunguko huo mrefu unawatesa Wanaileje wengi ambao hutaka kutembelea mgodi wao ama kwa kutalii ,mafunzo au kwa kazi maalum kwasababu tu ya miundombinu mibovu inayowalazimisha kupitia wilaya za Kyela na Rungwe, ambapo viongozi wa sasa wa wilaya hiyo wamesema inatosha wakichukua hatua za ujenzi wa barabara kupitia Ngulugulu na mkakati wa ujenzi wa daraja kule Landani.

Katika safari hiyo yapo mengi niliyoyaona na kupata maelezo juu ya uwepo wake nikiamini kwa pamoja tunaweza kuchukua hatua iwapo uwepo wake ni wa faida au  hasara.Tafadahali fuatilia mfululizo wa picha hizi na maelezo yake kwa ufupi.

Ni kwenye kilele cha Mlima Kaburo barabara ya Ndembo-Ileje kwenda Kyela 
Mmoja wa wavamizi wa msitu wa mlima Kaburo alinashwa na kamera yetu akiwa kwenye shughuli haramu ya uchomaji mkaa katika pori hilo



Uharibifu unaofanywa na wavamizi wanaochoma mkaa mlima Kaburo kunapunguza miti ya asili na kuharibu mandhari ya mlima huo 
Baadhi ya viongozi wa Halmashauri ya Walaya ya Ileje wakiwa ndani ya msitu wa  Kaburo kuangalia usalama wake


Uharibifu wa mazingira jinsi ulivyochangia kuharibu mandhari ya Mto Kiwila juhudi kubwa zinahitajika ili kurejesha hali yake 

 Lori aina ya Fuso (maarufu kama Mwalamusha) likipandisha Mlima Kaburo kutoka Kyela kwenda Ileje
Waweza kusema ni michezo ya kitoto katika maji kwa kutumia mashina ya migomba, hali haiko hivyo inasemekana njia hiyo ni ya kusafirisha mbao katika Mto Songwe wilayani Kyela mkoa wa Mbeya ambapo watu wazima huwatumia watoto kusafirisha mbao kwa kufungwa pamoja na mashina ya migomba kama kiini macho ili kukwepa ushuru pamoja na mkono wa serikali kwa ujumla 




 Upande wa Malawi unavyoonekana katika mpaka wa Kasumulu (border) wilayani Kyela
 Upande wa Malawi unavyoonekana katika mpaka wa Kasumulu (border) wilayani Kyela
 Biashara ya maembe Busale-Kyela ambapo ndo moja ilikuwa ikiuzwa Tzsh.1000

 Ramani ya mgodi wa Kiwila,mbele ni majengo ya utawala na kiwanda ,nyuma ni Mlima Kaburo ambao una zaidi ya tani milioni 30 za makaa ya mawe ambazo bado hazijachimbwa
 Moja ya viberenge au treni zilizokuwa zikibeba makaa ya mawe kikiwa kwenye njia yake(reli)
 Gari yaliyochakaa kwasababu ya kutelekezwa kutokana na kiwanda (mgodi) kusimama uzalishaji
 Mlango wa kuingia ndani ya mgodi wa Kiwila
 Moja ya mitambo iliyochakaa kutokana na kutofanya kazi kwa muda mrefu
 Sehemu ya uzalishaji umeme katika mgodi wa Kiwila
 Chumba cha kuongoza mitambo ya kuzalisha umeme mgodini hapo
 Ndani ya karakana ya mgodi ambapo ilikuwa ikizalisha vipuli (spea) mbalimbali za mitambo


 Jengo la utawa la katika mgodi wa Kiwila



 Moja ya majengo maarufu sana mgodini hapo.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni