Ijumaa, 6 Januari 2017

KAMATI YA ULINZI ILEJE KILA MMOJA KULEA MITI KUMI

 Mto Itumba ulivyofurika hadi kwenye mashamba ya wakazi wa kitongoji cha Kibanji katika kijiji cha Itumba

Na: Daniel Mwambene,Ileje
Katika kutimiza kwa vitendo zoezi la kila mwanafamilia kupanda miti kumi, wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ya Ileje mkoani Songwe kila mmoja amegawiwa miti kumi na kutakiwa kuwa mfano wa kuigwa katika kuitunza.

Akigawa miche ya miti katika viwanja vya ofisi za wilaya Mkuu wa Wilaya hiyo Mh. Joseph Mkude aliwataka wajumbe hao kuhakikisha kila mmoja wao anapanda miche hiyo na kuilea ili iweze kukua na kufikia hatua nzuri.

“Tutakuwa tunakagua miti yenu kwanza kisha kwa Wakuu wa Idara wote, Wah. Madiwani na wananchi wengine ambapo kila mwanafamilia anatakiwa kupanda na kuilea naagiza kila kiongozi kwenye ngazi yake ahakikishe anasimamia zoezi hilo”alisisitiza Mh,Mkude.

Katika mgao huo miche ya miti ya mbao,na kivuli iligawiwa kwa wajumbe hao ikiwa imenunuliwa na ofisi yake huku viongozi wa taasisi,makanisa na misikiti wakitakiwa kufanya hivyo.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa miche hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo aliahidi kulinda miti hiyo sanjali na kusimamia watendaji walio chini yake.

Huku hayo yakijili wakazi wa vitongoji vya Chafwonya na Kibanji katika kijiji cha Itumba baadhi yao wameonja  madhara ya kutoacha mita 60 toka kwenye mto zilizopo kesheria baada ya Mto 

Itumba kufurika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika kata za Ndola na wilaya ya Mbeya Vijijini ambako ni chanzo cha mto huo.

Uchunguzi wetu ulibaini mto huo kufurika hadi kwenye mashamba ambayo yamegharimu wakulima maelfu ya fedha za mbolea za chumvi chumvi.
 Mkuu wa Wilaya ya Ileje Mh.Joseph Mkude (kulia) akimgawia miche Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Haji Mnasi (kulia)
 Sehemu ya miche ya miti waliyokabidhiwa Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Ileje
Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wakiwa na sehemu ya miche waliyokabidhiwa na mwenyekiti wa Kamati hiyo Mh Joseph Mkude.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni